Jumanne, 28 Februari 2017

lijue kabila la WANYAMBO japo kwa ufupi

Wanyambo

Wanyambo ni kabila la Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Kagera, Wilaya ya Karagwe. Lugha yao ni Kinyambo. wanyambo pia nikabila ambalo lina utamadun tofaut na makabila mengine katika mkoa wa kagera tofauti zao kitamaduni -mavazi yaliyotumika kitamadunu yalifahamika kama (embugu)zilitokana na magome ya miti iitwayo kwa kinyambo "emitoma" Imetawaliwa na viongozi maarufu kama "omukama" na walio maarufu sana mpaka sasa hivi ni omukama Rumanyika na omukama Ruhinda Snr(balozi mstaafu) anayekaa makao makuu huko karagwe, Nyakahanga. Watu wengine wajulikanao ni familia ya Kazimoto walio ishi Nyakahanga karibu na kiongozi huyo wa jadi. Watu huwachanganya wanyambo na wahaya kwa kuwa wahaya wana majigambo na maneno mengi sana na hivyo kuelekea kumchanganya mnyambo na mhaya. Baadhi ya wanyambo wamechanganyikana na asili ya kinyarwanda kwa sababu wakimbizi waliishi karagwe na "kuintermarry" na watu wa karagwe. Wanyambo hupenda kula Ndizi kama chakula chao. Zamani ungemuuliza mnyambo halisi alichokula angesema "nalya amatoke" maana "nimekula chakula" ila kama alikula ugali angesema "tinalya akantu" maana "sijala chochote".